Michezo
Ezekiel Kamwaga awa Katibu Mkuu mpya wa Simba
Uongozi wa timu ya wekundu wa Msimbazi Simba ya jijini Dar es Salaam umemtangaza rasmi mrithi wa katibu mkuu wake wa zamani, Evodius Mtawala kuwa ni Ezekiel Kamwaga. Mtawala alipata kazi nyingine kama mkurugenzi wa kitengo cha wanachama na sheria TFF.
Ezekiel Kamwaga
Uongozi huo wa Msimbazi pia umemteua Asha Muhaji ambaye ni mwandishi wa habari za michezo kuwa afisa habari mpya wa klabu hiyo.
Asha Muhaji