Habari

Keko ‘kuchana’ mbele ya rais Museveni


Msanii wa kwanza wa kike wa hip hop kuwahi kufanikiwa nchini Uganda Keko, leo anatarajiwa kutumbuiza mbele ya rais Yoweri Museven na mke wake. Rais huyo atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa MaryHill High School Mbarara.

Mke wa rais Museveni, Janet Museveni alisoma katika shule hiyo ambapo Keko naye alisoma.
Asubuhi ya leo (June 23) ametweet, “MARYHILL High School Golden Jubilee Celebration Today ‪#CatchMeInYourCity‬ MBARARA HERE I COME ‪#KekonianArmy‬ Goodmorning.”

Msanii huyo kwa sasa wimbo ana wimbo aliomshirikisha Madtraxx wa Kenya uitwao “Make You Dance” unaofanya vizuri barani Afrika na Ulaya. Rapper huyo kwa sasa ni miongoni mwa wasanii wa kike wanaofanya hip hop waliofanikiwa zaidi barani Afrika.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents