Michezo

Kelvin John miongoni mwa vijana 60 watakaofanya makubwa duniani – The Guardian

Mchezaji wa Tanzania, Kelvin John ametajwa miongoni mwa vijana 60 wa kizazi kijacho wanaotarajiwa kufanya makubwa katika mchezo wa soka waliozaliwa mwaka 2003 duniani.

Kwa mujibu wa The guardian imemtaja mchezaji huyo ambaye wenyewe wamemuandika kwa jina lake la utani ‘Mbappe’

”Mbappe wa Tanzania, mtoto wa Juan Pablo, Tomás Ángel ni miongoni mwa wachezaji wetu waliyozaliwa mwaka 2003.”- The guardian

Kwa Afrika wametajwa wachezaji watano tu, Mcongoman Isaac Tshibangu,Prince Kwabena Adu wa Ghana,Mguinea Alaix Moriba,Mmoroco Mohamed Amine Essahel na Kelvin John.

Kelvin John kwa sasa yuko Brooke House of College huko Leicestershire Uingereza sasa ana miaka 16 atakapofikisha miaka 18 anatarajia kuianza rasmi safari yake ya soka la kulipwa barani ulaya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents