Habari

Kesi ya Abdul Nondo yatikisa Mahakama Kuu

Mahakama Kuu ya Tanzania imeahirisha kesi ya Abdul Nondo dhidi ya DPP, DCI na IGP mpaka tarehe 11, April mwaka huu ambapo itasikilizwa tena ambapo leo Jaji Rehema Sameji alipanga kutoa uamuzi.

Kulikuwa na mabishano ya pande zote mbili leo katika kesi hiyo ambapo Jaji Sameji aliahirisha kesi hiyo mpaka tarehe 4 ambapo Mahakama itaangalia kama itatoa maauzi au la!

Akiongea na Bongo5 leo, Mwanasheria wa Mtandao wa Wanafunzi, Paul Kisabo amesema kuwa “Leo tulifika Mahakama Kuu kwaajili ya kusikiliza kesi ya Abdul Nondo dhidi ya AG, DCI na IGP na Jaji Rehema Samuji alipanga kutoa uamuzi leo tarehe 4, April baada ya mabishano baina ya pande zote mbili leo katika Mahakama Kuu Mh. Jaji Sameji amesema kwamba amehairisha kesi mpaka tarehe 11 mwezi wa 4 ambapo itakuja kwaajili ya kusikilizwa na siku hiyo mahakama itaangalia kama siku hiyo itakuja kutoa tena maamuzi,” amesema Kisabo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents