Michezo
Kesi ya Aveva, Kaburu hali bado tete (Picha)
Kesi inayowakabili viongozi wa klabu ya soka ya Simba, Evans Aveva na Godfrey Nyange ‘Kaburu’ imekhairishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo na kutarajiwa kusikilizwa tena Agosti 30 mwaka huu.
Aveva na Kaburu wanakabiliwa na tuhuma za kughushi nyaraka za Simba SC na kutakatisha dola 300,000 (zaidi ya Sh milioni 650).
Kesi ya viongozi wa Simba yasogezwa mbele
Zifuatazo ni picha za matukio ya viongozi hao walipokuwa wakiwasili mahakamani
By Hamza Fumo na Yassini Ng’itu