Habari
Yajiyojiri kwenye kesi ya Kitilya na wenzake
Kesi ya aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, TRA, Harry Kitilya, aliyekuwa afisa mwandamizi benki ya Stanbic tawi la Tanzania, Miss Tanzania 1996, Shose Sinare pamoja na mwenzao Sioi Solomoni imesikilizwa leo.
Kesi hiyo ilitajwa kusikilizwa Jumanne hii katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam lakini imeahirishwa hadi Mei 18 kutokana na jalada la kesi hiyo ambalo lilitegemewa kurudi leo kutorudishwa. Watuhumiwa wamerudishwa tena rumande.
Aidha watuhumiwa walitakiwa kufika mahakama kuu kwa ajili ya kuendelea na rufani ambapo baada ya kufika mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imepanga kuanza kusikiliza rufani hiyo May 5.