Burudani
Oscar Pistorius kuendelea kukaa jela zaidi
Bodi ya parole nchini Afrika Kusini jana ilisogeza mbele kutolewa jela kwa Oscar Pistorius anayetumikia kifungo kwa kumuua mpenzi wake.
Bodi hiyo ilikutana jijini Durban mwezi uliopita lakini iliahirisha tena kesi yake kwa wiki mbili. Katika kipindi hicho idara ya haki ilisema haikupata muda wa kumaliza kesi ya Pistorius kutokana na kuwa na mambo ya kuyapitia.
Haijatangazwa lini bodi hiyo itakaa tena kusikiliza upya uamuzi wa parole.
Mwanariadha huyo mlemavu alifungwa mwaka jana baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp nyumbani kwake huko Pretoria kwenye Valentine’s Day, mwaka 2013. Hadi sasa ameshakaa jela kwa mwaka mmoja.
Awali alikuwa aachiliwe August 21 kuendelea na kifungo cha ndani.