Habari

Kesi ya malkia wa meno ya tembo kusikilizwa tena wiki ijayo

Kesi inayomkabili raia wa China, Yang Feng Glan (66) maarufu kama Malkia wa tembo inayosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam itaendelea kusikilizwa kuanzia Aprili 5 hadi 7, mwaka huu.


Yang Feng Glan, maarufu kama Malkia wa tembo

Wakili wa Serikali, Elia Athanas alidai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi, Huruma Shaidi kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kusikilizwa na kwamba mawakili wanaosikiliza kesi hiyo hawapo.

Hata hivyo, Wakili wa utetezi, Hassan Kiangio alidai kuwa kesi hiyo imeahirishwa kwa mara ya pili tangu mshitakiwa Manase Philemon (39) kudai amepigwa na kuteswa wakati akichukuliwa maelezo yake, ambapo upande wa mashitaka ulitakiwa kuleta mashahidi ili kuthibitisha tuhuma hizo.

Hatua ya upande wa mashitaka kuleta mashahidi ni kusikiliza kesi ndogo ndani ya kesi kubwa baada ya shahidi Sajenti Beatus (46) kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kudai kuwa aliandika maelezo ya mshitakiwa huyo na baadaye mshitakiwa kupinga kupokelewa kwa maelezo hayo kwa madai kuwa aliteswa na kupigwa.

Kiangio alidai kuwa mashahidi watakaoletwa na upande wa mashitaka watathibitisha ni kwa namna gani maelezo hayo yalichukuliwa. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 5 hadi 7, mwaka huu, kesi itakaposikilizwa mfululizo.

Mbali na mshtakiwa huyo, washitakiwa wengine ni Salvius Matembo (39) na Philemon (39). Watuhumiwa hao wanatuhumiwa kufanya biashara ya vipande vya meno ya tembo 706 vyenye uzito wa kg 18892 thamani yake ikiwa ni shilingi bilioni 5.4 bila leseni ya Mkurugenzi wa wanyama pori.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents