Habari

Kesi ya mke wa Bilionea Msuya yapigwa tarehe nyingine

Mahakama ya Hakimu Kisutu imeshindwa kuamuru kesi ya mauaji inayomkabili mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya na kuaihirisha tena hadi Februari 6 mwaka huu.

Hayo yametokea leo baada ya wakili wa serikali Kishenyi Mutalemwa kuieleza mahakama kuwa kesi hiyo ingesomwa kwaajili ya kutolewa maamuzi lakini Hakimu Mkazi Mkuu Godfrey Mwambapa anayesikiliza kesi hiyo alisema hawezi kusikiliza kesi hiyo kwasababu kuna barua kutoka kwa ndugu wa Msuya na anasubiri maelekezo.

Hakimu Mwambapa alitakiwa atoe hoja zinazowasilishwa upande wa utetezi pamoja na upande wa mashtaka ambapo wakili John Malya aliomba washtakiwa hao waachiwe huru kwasababu hakuna hati ya mashtaka inayowashikilia washtakiwa hao mahakamani hapo.

Kwa upande wake Wakili wa serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa aliiomba mahakama iwape muda ili waweze kutekeleza amri ya mahakama iliyotolewa Januari 9, 2017.

BY: Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents