Michezo
Kevin De Bruyne kukaa nje ya uwanja kwa wiki sita
Mchezaji wa Manchester City, Kevin de Bruyne, atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki sita baada ya kuumia goti siku ya Jumatano.
De Bruyne alipata jereha la goti la kulia katika mchezo wa kombe la Capital, ambapo Man City, waliwakabali Everton, na kushinda kwa mabao 3-1.
Wakala wa mchezaji huyu Patrick de Koster, amesema, “Nimezungumza na Kevin, amesema atarudi uwanjani kwa nguvu zaidi.”
Mchezaji huyo atakosa michezo muhimu ya timu yake ukiwemo ule wa fainali ya kombe la Capital, dhidi ya Liverpool, hapo Februari 28, pia atakosa mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi Dynamo Kiev.
Kulikua na wasiwasi huenda mchezaji huyo asingeweza rudi dimbani mpaka mwisho wa msimu