Burudani
Khadija Kopa, At, Berry Black, Ally Kiba na Diamond kula Eid Muscat
Wasanii watano leo saa tano asubuhi wamekwea pipa kwaajili ya kutimkia uarabuni Oman kwaajili ya kufanya show katika Ramee Dream Resort huko Seeb Muscat, kwaajili ya kutoa burudani katika sikukuu ya Eid ul-Fitr.
Wasanii ambao wanakadiliwa kuondoka ni mkongwe wa taarab nchini kutokea bendi ya ToT, Khadija Omari Kopa, At , Berry Black, Ally Kiba na Diamond ambaye mpaka wenzake wanaingia kwenye ndege kwaajili ya safari yeye alikuwa bado hajafika bila sababu maalum kujulikana.