BurudaniUncategorized

Khadija Kopa avifumbia macho vibeniten, kisa?

Msanii wa muziki wa taarab nchini, Khadija Kopa amesema moja ya vitu ambavyo havipendi ni kuwa katika mahusiano na mtu mdogo kwake kiumri.

Muimbaji huyo ameiambia Kikaangoni, EATVkuwa licha kutopenda jambo hilo lakini isiwe sababu ya kuwasema vibaya wanawake waliyo katika aina hiyo ya mahusiano.

“Mbona nyinyi wanaume wazee mnaoa wanawake wadogo na sisi hatusemi, sisi kila siku vibenteni vibenteni. Babu wee, mimi sipendi viben ten, mimi nilikuwa na mume wangu, na hata ikiwa dini yetu inaruhusu Mtume wetu alituonyesha njia,” Khadija Kopa.

Katika hatua nyingine Khadija Kopa ameongeza kuwa baada ya mume wake kufariki kipindi kirefu, yeye yupo tayari kuolewa ila na mtu mwenye umri wa kuanzia miaka 40 ila asizidi sana.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents