Burudani
Kifafa alichopata Chris Brown kilisababishwa na msongo mkubwa wa mawazo
Imebainika kuwa kifafa alichopata Chris Brown jana kilisabishwa na stress zinazomwandama kutokana na jinsi vyombo vya habari vinavyomwandika vibaya.
Jana TMZ waliripoti kuwa kitengo cha zima moto cha Los Angeles kilienda kwenye studio ya kurekodia muziki baada ya mtu mmoja kupiga 911 na kudai kuwa Chris alikuwa amepatwa na kifafa. Hata hivyo Chris aligoma kutibiwa.
Mwakilishi wa Chris anasema kifafa hicho kilisababishwa na uchovu mkali na msongo mkubwa wa mawazo na vyote vikitokana na kesi zinazomkabili na jinsi anavyoandikwa vibaya.
Baadaye Chris alitweet:
They won't love u until u r a memory…
— Chris Brown (@chrisbrown) August 10, 2013
‘Hawatakupenda hadi uwe kumbukumbu’