Habari
Kifahamu kiburi cha Liam Payne kumnunulia Wizkid champagne ya tshs bil 2.9 kwenye birthday yake
Unaweza kununua champagne ya kunywa siku moja tu yenye thamani ya paundi milioni 1.2 ambazo ni zaidi ya shilingi bilioni 2.9?
Kwa Liam Payne wa kundi la Uingereza la One Direction, hizo ni fedha za njugu tu na ndio maana hakuona hatari kumnunulia mshkaji wake Wizkid wa Nigeria champagne aghali zaidi duniani, Goût de Diamants aka ‘A Tribute to Luxury’.
Lakini kuna sababu kubwa ya kwanini kijana huyo aliamua kutumia kiasi hicho kikubwa cha fedha. Mwaka jana pekee Liam Payne aliingiza paundi milioni 5. Mwaka huu Kundi lake, One Direction limetajwa kwenye orodha ya mamilionea vijana walio chini ya miaka 30.
One Direction
Mwaka jana pekee, walipiga show zilizouza 60 na kuingiza paundi milioni 11.8.