Burudani

Kigezo cha kumsainisha Darassa record label

Msanii wa Bongo Fleva na hitmaker wa wimbo ‘Muziki’ ameweka bayana kigezo ambacho anaangalia iwapo mtu anamuhitaji kumsainisha katika lebo.

Rapper huyo ameeleza kuwa kwanza linapokuja suala la lebo ni biashara ambayo unapaswa kuridhia na kujua maslai yako wapi.

“Mtu kama mimi huwa sipiganii maslai yangu tu kwa sababu naamini ningekuwa napigania maslai yangu tu ningekuwa na mafanikio makubwa kuliko wasanii wengine wote kwa kitu ambacho nimekipata lakini huwa naangalia na watu wanaonizunguka kwa kuwa sifanyi hivi vitu pekee yangu,” Darassa ameiambia XXL ya Clouds FM na kuongeza

“Kwa hiyo kutoka kwenye lebo moja kwenda nyingine lazima niangalie na watu wanaoniamini, nimetembea nao safari ndefu lazima ni angali na wao watabaki katika nafasi gani kitendo cha mimi kuchukuliwa kwenda kusaini lebo nyingi.”

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents