Kili Tanzania Music Awards 2009

Image
Hatimaye Kili Tanzania Music Awards zilifikia kilele chake hapo jumamosi ndani ya Diamond Jubilee. Mkurugenzi wa Zizzou Fashion Bw. Tippo ambaye pia ni Meneja wa
mwanamuziki Mangwea alipokea tuzo kwa niaba ya msanii huyu kutoka kwa CEO wa Bongo5 Media
Group, Mangwea
ameshinda tuzo ya masanii bora wa Rap. Bofya hapa kuangalia video kibao.

Chingy akimkabidhi tuzo Chidi
Msanii kutoka Marekani Howard Bailey ‘Chingy’ alicheza ‘Ngoma Itambae’ kabla ya kumkabidhi tuzo Chidi Beenz kama msanii bora wa Hip Hop.

Kwa upande wa Jahazi Modern Taarab iliyo chini ya Mzee Yusuf walipata tuzo mbili moja ya wimbo bora ya taarab ambayo ni V.I.P na albamu bora ya taarabu ambayo pia ni V.IP.

Hoyce Temu akimkabidhi tuzo Nameless

Matonya alipata tuzo mbili ambazo ni wimbo bora wa kushirikiana uitwao ‘Anita’ na Wimbo bora wa Mwaka ambao pia ni ‘Anita’, ambao alishirikiana na Judith Wambura ‘Lady Jaydee’.

Wasanii wengine waliotwaa tuzo hizo ni Mwimbaji bora wa Kike iliyochukuliwa na Keysha wa Tip Top Connection, Mwimbaji bora wa Kiume alichukua M.B Doggy, Albamu Bora ya Taarabu ni V.I.P ya kundi la Jahazi.

Wimbo Bora wa Kiswahili (bendi) ni ‘Heshima kwa Mwanamke’ ya FM Academia, Albamu bora ya Kiswahili (bendi) ni Akudo Impact ‘Pekecha Pekecha’.

CPwaa akimkabidhi tuzo Hammi B

Orodha nzima ya washindi ni:

   1. Mwimbaji Bora wa Kike- Keisha
   2. Mwimbaji Bora wa Kiume- Mb Dogg
   3. Albamu Bora ya Taarab- VIP(Jahazi Modern Taarab)
   4. Wimbo Bora wa Taarab- VIP (Jahazi Modern Taarab)
   5. Wimbo Bora wa Mwaka- Anita (Matonya ft Lady JayDee)
   6. Wimbo Bora wa Kiswahili- Heshima kwa Mwanamke (FM Academia)
   7. Albamu Bora ya Kiswahili- Pekecha Pekecha(Akudo Impact)
   8. Wimbo Bora wa R& B- Natamani (Q Jay ft Makamua & Joslin)
   9. Albamu Bora ya Muziki Asilia- Dela Dela( Che Mundugwao)
  10. Wimbo Bora wa Hip Hop- Ngoma Itambae(Chid Benz)
  11. Wimbo Bora wa Reggae- Ripoti (Tunda Man)
  12. Msanii Bora wa Rap- Mangwea
  13. Wimbo Bora wa Afrika Mashariki- Salary(Nameless from Kenya)
  14. Mtunzi Bora wa Muziki- Karama Legesu
  15. Mtayarishaji Bora wa Muziki- Hammi B
  16. Mwandikaji Bora wa Muziki- Prof.Jay
  17. Wimbo Bora wa Zouk- Nalivua Pendo(Mwasiti)
  18. Mtayarishaji Bora wa Video- Kallaghe Production
  19. Wimbo Bora wa Collaboration- Anita (Matonya ft Lady Jaydee)
  20. Wimbo Bora wa Asilia- Kazi ya Dukani(Dogo Mfaume)

Bofya hapa kuangalia video kibao pamoja na tuzo zote….

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents