Kim Kardashian athibitisha hili na mumewe Kanye West (Video)
Ni kweli kabisa Kim Kardashian na mumewe Kanye West wanatarajia kupata mtoto wao wa tatu.
Hilo amelithibitisha Kim Kardashian katika msimu wa 14 wa kipindi cha Keeping Up With the Kardashians wakati akiongea na simu na dada yake Khloé.
“We’re having a baby!,” Kim amemwambia dada yake Khloe kwenye maongezi yao katika simu.
Season 14 is gonna be wild. Tune in this Sunday!!! #KUWTK pic.twitter.com/rnpIdGiNyK
— Kim Kardashian (@KimKardashian) September 28, 2017
Wakati huo huo familia ya Kardashian inatarajia kuwa kubwa zaidi ifikapo mwakani, ambapo wanatarajiwa kuwakaribisha watoto wengine ambao watazaliwa ukiachana na mtoto huyo wa tatu kutoka kwa Kim na mumewe Kanye West, wengine ni kutoka kwa Kylie Jenner na mpenzi wake Travis Scott, na Khloé na mpenzi wake Tristan Thompson.