Kiongozi maarufu wa upinzani Afrika Kusini, Julius Malema ataka bara la Afrika liungane na litumie lugha moja ya kiswahili (+video)
Kiongozi mkubwa nchini Afrika Kusini wa chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters (EFF), Julius Malema, amependekeza bara la Afrika Liungane na liwe na sarafu yake kama ilivyo Ulaya na kutumia lugha moja ya kiswahili ili kuepuka lugha za kikoloni ambazo zinatumiwa kututenganisha.
Malema amesema hayo jana Agosti 29, 2018 kwenye mkutano na waandishi wa habari ulioandaliwa na EFF kama sherehe ya miaka mitano tangu chama hicho kianzishwe, ambapo aliongelewa mambo mbalimbali ikiwemo ujumbe wa Rais wa Marekani kwenye mtandao wa Twitter kuhusu marekebisho ya sheria ya ardhi Afrika Kusini ambapo amesema bara la Afrika haliwezi kukubaliana na mtu kama huyo anayeona watu weupe wananyanyaswa.
“Lazima tukuze lugha moja ambayo itatumika kwenye bara zima. Madharani Kiswahili, kinaweza kukuzwa ili kitumike bara zima la Afrika,” amesema Malema.
Kwa upande mwingine Malema amesema kuwa ni vyema wazo la Marehemu Ghadafi la kuunganisha bara la Afrika lifufuliwe ili iwe rahisi kuwa na sarafu moja na hatimaye kuepukana na ukoloni mamboleo.
Akikazia kuhusu lugha za kigeni, Malema amesema lugha kama kifaransa, Kiingereza na Kireno zililetwa kutuchonganisha na kututenganisha ili tusiungane, kiurahisi hivyo haoni umuhimu wa lugha hizo kuendelea kusalia barani Afrika.
Hata hivyo amewaonya wanawake wa Afrika kuacha mara moja kuvaa mawigi kwani ni moja ya njia ya kuendeleza ukoloni, huku akidai kuwa Kenya ni taifa ambalo halijapata uhuru kamili kwani ni vibaraka wakubwa wa mataifa ya Ulaya.
https://youtu.be/-R6BvEz-ltk
Safi Sana Na Tutmie Pesa Moja
Hii ni picha yako ya zamani hebu tueleze kwa nini hivi sasa afya yako imekongoroka mno!
😐🙄🙄🙄😕😕😕😕🙁🙁😦
HAIWEZI KUWA KIRAHISI RAHISI KAMA ANAVYODHANI, NI NGUMU NA HAKITOTOKEA KITU KAMA HICHO, NEVER….!!
Good idea ingawa itakuwa ngumu sana.
Hapo kuna tabu sananaaa
Wazo nzuri ,ila inaweza kua ngumu kidogo kutekelezwa
Wazo nzuri sana ila itakua rahisi kama na kingreza kitakuwepo ili kiswahili kitafsiriwe kwa kingereza
maoni ya malema maziri sana kama wa rahisi hoto wa afrika bakubali
Well
Am appreciating his argument
kitu kizuri sana
good I dear but kiswaili no no no no we can’t us Kenyans may be Tanzania they will agree not in Kenya
Wozaaaaa
Kiswahili swaga bhn Ndo mpango Mzima
Point ya msingi
Anafanya mazoezi sasa
Watu kama hawa duniani asaivi wamebaki wachache Kama mim mmojawapo nikiwepo
Kwa pasport nitakubali lakini kwa hilo NO,haitowezekana.
Nauna fikiri luga ya Africa nigani? (Ipi)
sanatu