Uncategorized

Kiongozi wa juu wa Democrat ataka Trump aondolewe madarakani, ni baada ya ripoti ya uchunguzi dhidi ya Urusi

Siku moja baada ya kuchapishwa kwa ripoti ya mchunguzi maalum Robert Mueller juu ya ushawishi wa Urusi kwenye uchaguzi wa Marekani, viongozi kadhaa wa ngazi za juu kwenye chama cha Democrat wameanza kutoa wito wa kuondolewa madarakani kwa Rais Donald Trump.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la Ujerumani, Deutsche Welle. Elizabeth Warren, aliyetangaza nia ya kuwania urais kupitia chama hicho, ameandika kwenye mtandao wa Twitter kwamba ripoti ya Mueller imeonesha ukweli kwamba “Serikali hasimu ya kigeni iliushambulia uchaguzi wa 2016 kumsaidia Trump na mwenyewe aliupokea msaada huo, na baada ya kuchaguliwa akataka kuzuwia uchunguzi dhidi ya mashambulizi hayo.”

Warren amesema sasa ni jukumu la Baraza la Congress kuchukuwa hatua za kukataa matumizi mabaya ya madaraka ili kulinda heshima ya utawala wa sheria.

Hata hivyo, spika wa Baraza la Wawakilishi kutokea chama cha Democrat, Nancy Pelosy, amesema hatopigania kura ya kumuondoa madarakani, ikiwa hakupata hakikisho la uungwaji mkono wa wajumbe wa Republican.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents