Habari
Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe, Morgan Tsvangirai afariki dunia
Kiongozi Mkubwa wa upinzani nchini Zimbabwe, Morgan Tsvangirai amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Tsvangirai (65) alikuwa akisumbuliwa na saratani ya tezi dume na alikuwa akipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini.
Bw. Tsvangirai na chama chake cha Movement for Democratic Change (MDC) alikuwa mpinzani mkubwa nchini Zimbabwe chini ya utawala wa rais Robert Mugabe.