Michezo
Klabu ya Jiangsu Suning ya nchini China ya msajili Mbrazili Alex Teixeira
Kiungo mshambuliaji wa Brazili na klabu ya Shakhtar Donesk ya Ukraine Alex amejiunga na klabu ya Jiangsu Suning ya huko nchini China mchezaji huyo ambaye alikuwa anawindwa na Liverpool katika dirisha dogo la mwezi Januari.
Alex Teixiera kulia akiwa na agent wake Junior Mendonza
Taarifa za mtandao wa klabu ya Shakhtar Donesk zinasema kuwa Teixeira atajiunga na Jiangsu Suning kwa ada ya Euro milioni 38
Liverpool hawana nafasi tena ya kumsajili kiungo huyo mshambuliaji ambaye pia anaweza kucheza nafasi ya winga ya kushoto na kulia
Teixeira anaungana na Mbrazili mwenzie Ramires ambaye ametimka Chelsea hivi karibuni na atakuwa chini ya meneja ambaye ni beki wa zamani wa chelsea Dan Petrescu.