Michezo
Kocha aliye zipa ubingwa wa Kombe la Afrika Zambia na Ivory Coast awa kocha mpya wa Morocco
Kocha Mfaransa, Renard, ambaye ana umri wa miaka 47, amefanikiwa kushinda Kombe la Mataifa ya Afrika mara mbili, mwanzo akiwa na Zambia mwaka 2012 na baadaye akiwa na Ivory Coast mwaka 2015, Herve Renard ameteuliwa kuwa kocha wa Morocco akirithi mikoba ya mzalendo,Badou Zaki aliyeondolewa wiki iliyopita.
Renard ameweka wazi mipango katika timu ya taifa ya Morocco mara tu baada ya uteuzi huo.
“Changamoto ya kwanza ni, kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2017, Na kufuzu kwa Kombe la Dunia mwaka 2018, hivyo ni ratiba muhimu mno,”amesema Mfaransa huyo.