Michezo

Kocha Sven afunguka kuhusu Kagere

Kocha wa Klabu ya Simba, Sven Ludwig Vandenbroeck amesema kuwa hana tatizo na mchezaji wake Meddie Kagere kama inavyodaiwa.

Sven amesema kuwa hawezi kutumia nguvu katika mambo yasiyokuwa na maana na wala asiyojua asiyojua yanapotokea.

“Siwezi kutumia nguvu kwenye mambo yasiyo ya maana ambayo sijui yanatoka wapi. Mimi sina tatizo, Medie hana tatizo hilo ndilo ninaweza kusema.”- Kocha Mkuu Sven Vandenbroeck

Kumekuwa na taarifa zinazoenea kuwa kocha huyo Mbelgiji na mshambuliaji wake Meddie Kagere hawana maelewano mazuri jambo ambalo kwa upande wake amelikanusha.

IMEANDIKWA NA HAMZA FUMO, INSTAGRAM @fumo255

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents