Kocha wa Chelsea afanya jitihada za kuwabakiza wachezaji hawa Chelsea
Kocha wa Chelsea afanya jitihada za kuwabakiza wachezaji hawa Chelsea
Baada ya kutambulishwa na Chelsea kama kocha mkuu Maurizio Sarri ameomba kukutana na hawa wachezaji ili kuogelea mwelekeo wao katika kikosi chake ambacho ameanza kukisuka.
Sarri ameomba kukutana na wachezaji wawili raia wa Ubelgiji ambao ni Eden Hazard pamoja na mlinda mlango wa timu hiyo Thibaut Courtois ambao wameripotiwa kuwa wanaweza kujiunga na klabu ya Real Madrid ambao inasemekana wametenga mkwanja mrefu unaokadiriwa kufika Euro mil 300.
Wachezaji hao wako mapumziko baada ya kumalizika kwa michuano ya kombe la Dunia nchini Urusi na kufanikiwa kuisadia timu yao ya taifa kuwa washindi watatu katika michuano hiyo.
Sarri alisema “Wachezaji mnaowaelezea ni wachezaji wa kiwango cha juu sana na ningependa kuwaweka katika kikosi changu”
aliongeza “Ningependa kukutana na wachezaji hawa uso kwa uso, kuzungumza nao na kuelewa nini jambo bora zaidi la kufanya hii ni kwa kila mmoja”
” Hazard ni mchezaji wa kiwango cha juu sana. ni mmoja miongoni mwa wachezaji wawili au watatu bora barani Ulaya”
lakini pia ameomba kama itawezekana wachezaji hawa wajiunge na timu yake kwa ajili ya mazoezi ndani ya siku nne au tano.
Klabu ya Chelsea ilishika nafasi ya tano katika msimmo wa ligi kuu nchini Uingereza msimu uliopita na imekosa sifa za kushiriki michuano mikubwa barani Ulaya ya UEFA Champions League,lakini pia ilifanikiwa kushinda taji la FA Cup kwa ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Manchester United,hivyo mchezo wa ufunguzi watacheza dhidi ya Mabingwa wa ligi hiyo ambao ni Manchester City.