Michezo
Kocha wa England baada ya kutolewa Euro 2016 ametangaza kujiuzulu
Kocha wa timu ya taifa ya England Roy Hogdson ametangaza kujiuzulu kuifundisha timu ya taifa England, kutokana na kupoteza mchezo wao wa 16 bora dhidi ya Iceland taifa lenye wakazi wasiozidi 330,000 huku ikiwa nafasi ya 34 kwenye viwango vya FIFA, kwa kufungwa goli 2-1, England walianza kupata goli la uongozi dakika ya 4 kwa mkwaju wa Penati kupitia kwa Wayne Rooney.
Dakika mbili baadae baada ya England kupata goli la uongozi, Iceland walisawazisha kupitia kwa Ragnar Sigurdsson dakika ya 6 na Kolbeinn Sigposson dakika ya 18.
Roy Hodgson ametangaza uamuzi huo wa kujiuzulu kuendelea kuifundisha England, ikiwa ni siku tatu zimebakia mkataba wake umalizike.