Michezo

Kocha wa Manchester United Ole Gunnar atoa kauli hii baada ya kupangiwa na Barcelona UEFA “Wakizembea tutawafanya kama tulivyowafanya PSG”

Leo mchana droo ya robo fainali ya Klabu bingwa barani Ulaya imepangwa, ambapo klabu ya Manchester United ya Uingereza imepangwa na Barcelona ya Hispania kwenye hatua hiyo.

Man United ndio wakaoanzia nyumbani Old Trafford kati ya tarehe 9/10 Aprili 2019. Tazama droo yote hapa chini. Droo hiyo, pia imepangwa na hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo, ambapo mshindi kati ya Barcelona na Man United atacheza nusu fainali na mshindi kati ya Liverpool na FC Porto. Mshindi atakayepita kati ya Man City na Spurs atacheza dhidi ya Ajax na Juventus.

Na baada ya makundi hayo kupangwa leo kocha wa Manchester United Mnorway Ole Gunnar ameongea haya baada ya timu yake kupangiwa na FC Barcelona:- “”Tunataka michezo kama hii dhidi ya klabu kubwa na timu kubwa,” anasema Ole. “Tulikutana mara ya mwisho dhidi yao mwaka 2009 na 2011 na nusu ya mwisho mwaka 2008 wakati Scholesy alifunga goli, ni michezo kama hii mashabiki wetu na klabu yetu inazitamani sana na Tulitarajia hii. “

Aliongeza “Mimi inawezekana nina asilimia 99 ya kuwa kocha wa muda wote hapa, na napendelea zaidi kama tulivyokutana na na PSG. Ikiwa wataweza kupata matokeo mazuri nyumbani, basi tunajua tunaweza kwenda na kuumiza mtu yeyote kama tulivyofanya huko Paris. “

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents