Michezo
Kocha wa Uholanzi Louis van Gaal akubali kuinoa klabu ya Manchester United
Kocha wa timu wa taifa ya Uholanzi Louis van Gaal amekubali kuwa kocha ya kudumu wa klabu ya Manchester United kwa mkataba mfupi usiozidi miaka mitatu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mtandao wa Goal zinasema Van Gaal amekubali kukinoa kikosi cha Manchester United na kwa mkataba mfupi usiozidi miaka mitatu na atakichukua kikosi hicho baada ya kumalizika kwa Kombe la Dunia itanayotajia kuanza mwezi ujao huko Brazil.
Taarifa hiyo imeendelea kusema kuwa Makamu mwenyekiti wa Manchester United Ed Woodward pamoja na moja ya wamiliki wa klabu hiyo wamekuwa kwenye mazungumzo na kocha huyo.
Pia taarifa hiyo imesema United ajaweza kuweka wazi uvumi huo na kudai kuwa United bado wapo kwenye makubaliano toka pande zote mbili.
Source:Goal