Kocha wa Uingereza, Southgate atamba hadharani ‘Nilijua tu nitamfunga Colombia’
Meneja wa Uingereza, Gareth Southgate ametamba kuwa alitambua tu timu yake ingeibuka na ushindi kwenyenmchezo wao dhidi ya Colombia.
Baada ya kutoka sare ya bao 1 – 1 katika dakika 90 za mchezo kwa bao la Harry Kane na la kusawazisha la Mina, hatimaye Uingereza imefanikiwa kusonga mbele kwenye hatua ya robo fainali ya michuano hiyo ya kombe la dunia kwa kuifunga Colombia jumla ya penati 4 – 3.
Najivunia kwa namna timu yangu ilivyo cheza, nadhani tuliweza kuutawala mchezo ndani ya dakika zote 90. Wachezaji wangu walicheza kwa nidhamu kubwa na kwa ushirikiano wa hali ya juu na hakika ulikuwa na mvuto kwa kundi hili la vijana na ulikuwa usiku maalum kwa kila mtu.
Uingereza itakutana na Sweden kwenye mchezo wa robo fainali huku timu hizo zikiwa zimekutana mara 15 na vijana wa Southgate kuibuka na ushindi mara mbili pekee.