Michezo

Kocha wa Ujerumani Joachim Low aikimbia Arsenal

Kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani, Joachim Low ameongeza mkataba wake wa kuendelea kuifundisha timu hiyo mpaka ifikapo 2022.

Rais wa shirikisho la soka nchini humo Reinhard Grindel amethibitisha kocha huyo kuongeza mkataba huo ambao ulikuwa unafikia tamati 2020.

Hata hivyokupitia mtandao wa Twitter wa shirikisho hilo wameongeza kwa kuandika, “OFFICIAL: Joachim #Löw has extended his contract as #DieMannschaft head coach until 2022! ✍️ #Löw2022.”

Kocha Low alikuwa anatajwa kurithi kiti cha mzee Arsene Wenger kwenye klabu ya Arsenal.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents