Michezo
Kocha wa Ujerumani Joachim Low aikimbia Arsenal
Kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani, Joachim Low ameongeza mkataba wake wa kuendelea kuifundisha timu hiyo mpaka ifikapo 2022.
Rais wa shirikisho la soka nchini humo Reinhard Grindel amethibitisha kocha huyo kuongeza mkataba huo ambao ulikuwa unafikia tamati 2020.
Hata hivyokupitia mtandao wa Twitter wa shirikisho hilo wameongeza kwa kuandika, “OFFICIAL: Joachim #Löw has extended his contract as #DieMannschaft head coach until 2022! ✍️ #Löw2022.”
OFFICIAL: Joachim #Löw has extended his contract as #DieMannschaft head coach until 2022! ✍️ #Löw2022 pic.twitter.com/WLu21vTpCW
— Germany (@DFB_Team_EN) May 15, 2018
Kocha Low alikuwa anatajwa kurithi kiti cha mzee Arsene Wenger kwenye klabu ya Arsenal.