Kocha wa West Brom afutwa kazi
Mkufunzi wa klabu ya West Brom ya nchini Uingereza, Tony Pulis amefutwa kazi na klabu hiyo kutokana na klabu hiyo kuwa na matokea mambaya.
Klabu hiyo kwa ina pointi moja tu huku ikuwa juu ya eneo la kushushwa daraja mbali na kutopata ushindi hata mmoja katika mechi zake 10 ilizocheza.
West Brom walicharazwa mabao 4 kwa sufuri na mabingwa watetezi wa ligi Chelsea.
Albion waliwezahinda mechi zake tatu za kwanza msimu huu lakini wameweza kutoka sare mechi nne na kupoteza saba tangu ilipoishinda Accrington katika kombe la Carabao 22 mwezi Agosti.
Aliyekuwa mkufunzi wa zamani wa klabu hiyo Gary Megson ambaye alikuwa naibu wa Pulis anachukua mahala pake hadi timu hiyo itakapotoa tangazo jingine.
“We are in a results business,” Alisema Mwenyekiti wa West Brom John Williams na kuongeza s“and over the back end of last season and this season to date, ours have been very disappointing.”
Tuko katika biashara ya kupatamatokeo mazuri lkini kutokana na matokeo mabaya ambayo yamekuwa yakishuhdiwa kufikia mwishoni mwa msimu uliopita na kufikia sasa matokeo yamekuwa mabaya.
West Brom inakutana na Tottenham ika ligi ya Uingereza katika uwanja wa Wembley siku ya Jumamosi.