Michezo
Kombe la Dunia: Nigeria yarudisha matumaini ya Afrika kwa kuingia hatua ya 16
Nigeria jana imekuwa timu ya kwanza ya Afrika kuingia hatua ya 16 ya kombe la dunia licha ya kufungwa 3-2 na Argentina kwenye uwanja wa Beira-Rio huko Porto Alegre.
Nigeria, ambao wameingia hatua hiyo ya mtaono kwa mara ya kwanza tangu 1998, watakutana na Ufaransa Jumatatu ijayo. Unahisi Nigeria wanaweza kufika fainali?