Michezo

Kombe la Dunia: Uholanzi yaiadhibu Hispania mabao 5-1, Van Persie na Robben wang’ara

Mabingwa watetezi wa kombe la dunia, Hispania wamerudishwa darasani na Waholanzi waliokuwa na hasira ya kulipiza kisasi cha kufungwa kwenye fainali ya mwaka 2010 kwa kupokea kichapo cha aibu cha mabao matano kwa moja.

article-2657446-1EBEA0A600000578-893_634x404

Katika fainali ya mwaka 2010, Andres Iniesta alifunga goli katika dakika za nyongeza na kuifanya ishinde bao 1-0 na kuchukua kombe la dunia nchini Afrika Kusini. Bao la kwanza na la pekee la Hispania lilifungwa na Xabi Alonso katika dakika ya 27 kupitia penalty.

Robin Van Persie alisawazisha goli dakika 44 ya kipindi cha kwanza kwa kichwa cha kupaa angani kilichowagusa wengi.

article-2657446-1EBE7DA400000578-813_634x371

Dakika ya 53 Arjen Robben alipachika bao la 2, kabla ya Stefan de Vrij kuweka jingine katika dakika ya 64. Van Persie aliongeza la nne katika dakika ya 72 kabla ya Robben kupiga msumari wa mwisho dakika ya 80 na kufanya mabao yawe 5-1.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents