Habari

Kongamano la Kiswahili lasisitiza umuhimu wa kuikuza lugha hiyo

Naibu waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Susan Kolimba,amewataka wataalamu wa lugha ya Kiswahili kuendelea kukuza lugha hiyo katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki.

suzani-kolimbaa

Ameyasema hayo katika kongamano la chama cha Kiswahili la Afrika, lilifanyika katika chuo kikuu cha Dar es Salaam, alipokuwa mgeni rasmi wa kongamano hilo.

“Nawapongeza kwa jihihada mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na chuo kikuu cha Dar es Salaam, katika kuikuza lugha ya Kiswahili, niwaombe wataalam wa lugha ya Kiswahili kuchangamkia fursa za fani hiyo kwa nchi za Afrika Mashariki,” alisema Kolimba.

Kongamano hilo lilihudhuriwa na wawakilishi kutoka nchi za Afrika Mashariki, mabalozi,wabunge, na balozi wa Kiswahili Afrika ambaye ni mke wa rais wa awamu ya nne Mama Salma Kikwete.

BY: EMMY MWAIPOPO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents