Habari

Korea Kusini yapanga kumuua kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un

Korea Kusini imejipanga kumuondoa duniani kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un iwapo itahisi kutishwa na shambulio la silaha kinyuklia, waziri wa ulinzi wa nchi hiyo amesema, CNN imeripoti.

160923132448-kim-jong-un-smiling-field-130916-exlarge-169

Alipoulizwa bungeni kama kuna jeshi maalum lililo tayari kumuua Kim Jong Un, Han Min-koo alisema: “Ndio, tuna mpango huo.” “Korea Kusini ina mpango wa jumla kutumia silaha nzito kulenga miundo mbinu ya adui katika maeneo makubwa pamoja na kuuondoa uongozi wa adui,” aliongeza.

Kwa muda sasa kulikuwepo na tetesi za kuwepo mpango huo lakini jibu hilo la wazi la waziri huyo limewashtua wengi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents