Habari

Kuanguka kwa Mugabe: Walinzi 27 wasimamishwa kazi

Kwa mujibu wa gazeti la The Standard la nchini Zimbabwe walinzi 27 wanaomlinda Rais Robert Mugabe wamesimimishwa kazi kwa kudaiwa hawakuwa wamejipanga baada ya rais huyo mzee kuanguka.

zimbabwe-dictator-mugabe-falls-down-steps-photographers-forced-to-delete-images

Kwa mujibu wa vyanzo, walinzi hao walipewa barua za kusimamishwa kazi Ijumaa iliyopita. Kuna ripoti pia kuwa baadhi ya maofisa wanaweza kufukuzwa kazi.

Sura mpya za walinzi wake zilionekana Ijumaa wakati Mugabe alipokutana na rais mpya wa Zambia Edgar Lungu mjini Harare.

Uchunguzi mkali unaendelea kufuatia tukio hilo lililomuabisha Mugabe.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents