Michezo
Kuelekea mchezo wa fainali ya kombe la Ligi UK Kolo Toure amuonya Yaya Toure
Mchezaji Kolo Toure ambaye ni mchezaji wa Manchester City atakabiliana na nduguye Yaya Toure wakati ambapo Liverpool itakutana na Manchester City katika fainali ya kombe la Ligi ya Uingereza siku ya jumapili katika uwanja wa Wembley.
Kolo Toure ambaye ni beki wa Liverpool anasema kuwa atatumia kila njia kuhakikisha kuwa ndugu yake huyo hapati bao
‘Ananijua mie kwamba naweza kutumia kila njia kumzuia asifunge bao”,alisema Kolo Toure ambaye ni ndugu mkubwa wa Yaya Toure.