Burudani

Kuhusu bidhaa za Juma Nature ‘Ndala’ kutoingia sokoni

Msanii mkongwe wa Bongo Flava, Juma Nature ameeleza ni kwa nini hadi sasa bidhaa zake za ndala hazijaingia sokoni.

Hapo awali msanii huyo alijidai kuwa angekuja na bidhaa hizo lakini hadi sasa hakuna alichotekeleza. Akizungumza na Planet Bongo ya EA Radio amesema ameamua kusitisha mpango huo.

“Unajua kila jambo ukilianzisha watu wengine wanaangalia ulichosema wewe ndio wanakaa wakifanye, hivyo nikaamua niache,” amesema Juma Nature.

Baadhi ya wasanii wamekuwa wakiingiza bidhaa zao sokoni, Weusi wameuza t-shirt, pensi na kufia kupitia brand yao ya Nyeusi, Jux amefanya hivyo kupitia brand yake ya African Boy na Diamond ameingiza bidhaa mbali mbali ikiwepo Chibu Perfume.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents