Burudani

Kuna msanii mkubwa hakupenda mimi kujiunga na WCB – Rich Mavoko

Msanii mpya kutoka lebo ya WCB, Rich Mavoko amesema kuna msanii mkubwa bongo alimkataza kujiunga na WCB.

13266823_882952098517543_720315630_n

Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo, kinachoruka kupitia EA Radio, Rich Mavoko amesema kuna msanii mkubwa alimtumia ujumbe wa simu na kumuuliza kwanini amekubali kwenda kusimamiwa na Diamond.

“Sijawahi kusema hili ila ukweli ni kwamba wakati nataka kwenda WCB kuna msanii mkubwa alinitumia ujumbe na kuniambia Rich Mavoko unakwendaje kusimamiwa kazi zako na Diamond Platnumz, kiukweli aliniumiza sana ila nilimjibu kwa roho moja kuwa brother wewe hujui mimi nimetoka wapi na nakwenda wapi hivyo huwezi kujua hata hili litakujaje kwangu,” aliongeza.

Rich Mavoko amekuwa juu tangu alipojiunga na lebo hiyo ya WCB na kuachia wimbo wake ‘Ibaki Story’ unaozidi kufanya vizuri kwenye TV na Radio.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents