Michezo

Kuna taarifa zinasambazwa mchezaji wetu ni Mrundi ili wa Djibouti wakate rufaa – Manara

Ofisa habari wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema kuwa kuna taarifa za upoteshwaji kwa baadhi ya watu wakidai kuwa mchezaji wa timu hiyo, Poul Bukaba ni raia wa Burundi na kuwataka wa Djibout kuikatia rufaa timu hiyo swala ambalo halina ukweli wowote.

 

 

 

Tunazo taarifa za hovyo zinazosambazwa eti mchezaji wetu huyo ni Mrundi na hvyo tutakatiwa rufaa dhidi ya Wadjibout.. Poul Bukaba @bukaba_paul ni mtanzania na Urundi alienda kucheza Soka tu na anamiliki uraia wa kuzaliwa wa Tanzania…tafuteni lingine hili mmenoa na pia hangaikeni na yenu ikiwemo kulipa mishahara ya wachezaji wenu….Ndegelec

 

Kikosi cha Simba SC kipo njiani kurejea Tanzania kikitokea nchini Djibouti katika mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Gendarmerie ambapo timu hiyo imefanikiwa kusonga mbele kwa jumla ya magoli 5 – 0 .

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents