Michezo
Kurt Zouma kukaa nnje mda mrefu
Beki wa kati wa Klabu ya Chelsea, Kurt Zouma amepata majeraha ya goti lake upande wa nyuma baada ya kutua vibaya wakati akirejea chini alipokuwa akiwania mpira wa juu katika mechi dhidi ya Man United iliyoisha kwa sare ya bao 1-1.
Beki huyo bado haijajulikana atakuwa nnje kwa mda gani lakini anaweza akakaa nje ya uwanja kwa muda mrefu na tayari wachhezaji wengine wakianza wa Man United, wamekuwa wakimliwaza.
Mchezaji Juan Mata, alimfuata palepale uwanjani na Marouane Fellaini alikuwa wa kwanza kumpa pole baada ya mechi kwisha, na beki Luke Shaw ambaye pia ni majeruhi pia alitupia mtandaoni akimuombea apone haraka.