Michezo
Kuyt aikataa Liverpool
Striker wa Liverpool anayetokea Uholanzi,Dirk Kuyt,ameitamkia klabu yake kuwa anataka kuondoka na kumfuata kocha wake wa zamani Rafa Benitez anayeinoa Inter Milan,huku dau lake likidaiwa kuwa ni paund milioni 13.
Japokua kocha wa Liverpool Roy Hodgson amwonyesha kutokubaliana na uwamuzi huo wakala wa mchezaji huyo Rob Jansen anadaiwa tayari kufanya mazungumzo na Inter.
Hodgson anakabiliana na wakati mgumu kutokana na kiungo mwingine Janier Mascherano naye kutaka kuondoka kwenda Barcelona au Inter.