Burudani
Kylie Jenner akanusha taarifa za kuachana na Tyga
Mrembo wa familia ya Kardashians, Kylie Jenner amezungumzia kuhusu taarifa zilizosambaa wiki iliyopita kuwa amempiga chini rapper Tyga ambaye ni boyfriend wake.
Akizungumza katika kipindi cha The Ellen Show, Kylie amekanusha kuhusu uvumi huo na kusema kuwa watu walielewa vibaya lakini yeye na Tyga hawajaachana.
“Honestly, people have it all wrong, We’re not broken up. We became best friends before anything happened, so I think that that’s awesome and we’re just like, hanging out.”
Baada ya kusema hayo Ellen alimuuliza alimaanisha nini kusema “HANGING OUT”, na Kylie akajibu “We’re still together.”
Wiki iliyopita TMZ iliripoti kuwa Kylie amempiga chini Tyga kutokana na shinikizo kutoka kwa familia yake.