Burudani
Kylie Jenner ampiga chini Tyga kwenye birthday yake
Couple ya mrembo Kylie Jenner na rapper Tyga inasemekana imevunjika.
Kwa mujibu wa TMZ, couple hiyo imevunjika baada ya kutokea ugomvi mkubwa ambao Tyga ndio chanzo.
Kylie amempiga chini Tyga siku ya Alhamisi NOV.19, siku ambayo Tyga alikuwa akisherehekea birthday yake ya 26 na marafiki mbalimbali wakiwemo A$AP Rocky, Wiz Khalifa, Jamie Foxx na Leonardo DiCaprio, lakini Kylie hakuonekana, wala yeye na dada zake hawakum-wish happy birthday kwenye mitandao ya kijamii.
Vyanzo vingine vimesema kuwa Kylie amemuacha rapper huyo kutokana na shinikizo kutoka kwa familia yake ya The Kardashians.
Tyga na Kylie ambao wamekuwa kwenye uhusiano kwa zaidi ya mwaka mmoja, hivi karibuni walionekana pamoja kwenye video mpya ya Tyga “Dope’d Up”.