Kylie Jenner amesema aliamua kuongeza ukubwa wa lips zake kwasababu hakuwa akijiamiani.
Mrembo huyo mwenye miaka 19, ameliambia jarida la Complex kuwa alikuwa na wasiwasi kuhusu wavulana kumbusu kwasababu aliona kuwa lips zake zilikuwa nyembamba mno.
“Huo umekuwa ni wasiwasi katika maisha yangu yote,” alisema.
Alikumbushia kwenye mahojiano hayo jinsi mvulana aliyekuwa anasoma naye alivyomuambia kuhusu lips zake. “Huyu mvulana niliyembusu alisema ‘Lips zako ni ndogo sana lakini unabusu vizuri.’ Sikudhani utakuwa mzuri katika kupiga busu.”
“Iliniuma sana,” alisema Kylie. “Kuanzia hapo, nilianza kuhisi kama naona wanaume wakiangalia lips zangu. Nilihisi kama hakuna mwanaume ambaye angenibusu.”