La Liga: Barcelona yapewa nafasi ya dharura kusajili safu ya ushambuliaji licha ya dirisha kufungwa
La Liga: Barcelona yapewa nafasi ya dharura kusajili safu ya ushambuliaji licha ya dirisha kufungwa
Klabu ya Barcelona imepewa nafasi maalumu na Chama cha soka nchini Hispania La Liga ili kuweza kuongeza mshambuliaji ndani ya siku 15 zijazo ikiwa ni nje ya utaratibu wa dirisha la usajili kwa wachezaji.
Maamuzi hayo yamekuja mara baada ya mshambuliaji wa klabu hiyo raia wa Ufaransa, Ousmane Dembele akitarajiwa kuwa nje kwa miezi sita kufuatia kupata jeraha.
Nafasi hiyo ya Barcelona kuongeza nyota mpya hataka kama dirisha la usajili limefungwa inakuja kutokana na sheria za La Liga kuruhusu klabu yoyote kusajili mchezaji kama tu itakosa huduma ya mchezaji wake kwa muda wa kipindi cha kuanzia miezi mitano.
Kwa mujibu wa La Liga wachezaji watakao sajiliwa lazima wawe wamewahi kucheza nchini Hispania au wachezaji huru. Hata hivyo wachezaji hao hawataruhusiwa kushiriki michuano ya UEFA.
Mpaka sasa Barcelona imempoteza nyota wake raia wa Uruguay, Luis Suarez kwa kuwa nje ya uwanja kwa miezi minne tangua Januari kabla ya Dembele kupata majeraha.
Imeandikwa na Hamza Fumo