Habari

Lady Gaga ahudhuria party na mavazi ya Bibi Harusi


Picha hii isikuchanganye. Lady Gaga hakuolewa siku ya Jumapili bali aliamua tu kutoka kivyake kwa kuvaa shela kama bibi harusi kwenye party jijini London.

Gaga, akiwa na Jay-Z na Rihanna, walisababisha shangwe kubwa baada ya wote kuhudhuria kwenye sherehe za baada ya michezo ya Paralympic Games kwenye klabu ya Arts, ya London, Uingereza.

Gaga kama kawaida yake aliwashangaza wengi, baada ya kutoka kwenye gari akiwa na muonekano wa bibi harusi wakati Rihanna aliamua kutoka simple tu kwa kupiga pajama nyekekundu na jaketi la ngozi.

Mapema usiku huo, Rihanna aliungana na washkaji zake wa kundi la Coldplay na kuangusha bonge la performance wakati wa ufungwaji wa Paralympic Games.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents