Habari
Lady Gaga anunua ‘wheelchair’ yenye dhahabu tupu
Siku zote Lady Gaga hupenda kuwa tofauti na kwa kuthibitisha hilo, amenunua baiskeli ya walemavu yenye dhahabu tupu iliyobuniwa na Ken Borochov kwaajili ya brand ya Louis Vuitton ambayo alionekana nayo mitaa ya Chicago jana.
Hiyo ilikuwa ni zawadi yake mwenyewe kwa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza miaka 27 hiyo jana.
Gaga amekuwa akitumia wheelchair tangu February, baada ya kupata tatizo kwenye hips na hivyo kulazimisha kusitisha ziara yake ya Born This Way Ball na hatimaye kufanyiwa upasuaji.
Pamoja na kuwa mgonjwa, Lady Gaga ameendelea kuipromote perfume yake ya FAME. Pia albam yake ijayo iitwayo ARTPOP, itapatikana kwa awamu mbili miezi kadhaa ijayo.