Burudani
Lady Jaydee ajipanga kufanya ziara ya Afrika
Malkia wa Bongo Fleva, Lady Jaydee amepanga kuanza ziara yake ya kimuziki katika bara la Afrika.
Jaydee amthibitisha hilo kupitia ujumbe wake ambao ameuandika kwenye mtandao wa Instagram.
“Nataka kufanya Africa Tour 🗺 |Siku zote kabla hujaanza kitu unafikiria kukwama na kujiuliza je! Utaweza ?,” ameandika Jide kwenye mtandao huo.
Kwa sasa Msanii huyo anafanya vizuri na wimbo wake ‘Anaweza’ ambao amemshirikisha msanii mkongwe wa Jamaica, Luciano.