BurudaniLady Jay Dee
Lady JD aporwa
Habari za kusikitisha zilizofika dawatini ni kuporwa kwa mkoba wa mwanamuziki Lady JD. Tukio hilo la kusikitisha lilitokea usiku kwenye uwanja wa taifa wakati timu ya soka ya taifa ilipomenyana na Ivory Coast kwenye mechi ya kirafiki. Ishu ilikuwa wakati akitoka akiwa na marafiki zake, miongoni akiwepo mlinda mlango maarufu wa Simba, Juma Kaseja ambapo inadaiwa kundi la vibaka wakiwa na bisibisi na mapanga liliwavamia wakati wakielekea kwenye maegesho ya magari na kupora mkoba huo. Haijafahamika bado thamani ya vitu vilivyokuwemo ndani ‘kipima joto’ hicho