Burudani
Lamar aeleza kwanini haishi na mwanae wa kike mwenye miaka 8!
Lamar ana mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minane aitwaye Nisha.
Akiongea hivi karibuni kwenye kipindi cha Chill na Sky, Lamar alisema haishi na mwanae kwakuwa yupo nje ya nchi.
“Mimi mtoto wangu alikuwa hakai sana na mimi na mama yake alikuwa anaishi Canada sasa hivi yupo Marekani. Huwa anakuja wakati wa likizo tu,” alisema.
Lamar aliongeza kuwa kuwa na mtoto kumemfanya awe makini katika matumizi ya fedha.
“Inakufanya unakuwa na discipline ya matumizi ya hela. Kila unachopata unajua kabisa I have a family behind me,” alisema.